Peter Okoye wa P Square
aweka wino wa kuwa balozi
wa kampuni nyingine kubwa
duniani!
Mmoja ya wasanii wanaounda kundi maarufu la P Square kutoka Nigeria, Peter Okoyeanaziandika headlines baada ya taarifa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa staa huyo wa muziki Africa amedondosha wino kuwa balozi mpya wa kampuni ya viatu yaAdidas.
Ukichukuwa time na kutembelea social networks za Peter Okoye yani Twitter naInstagram utakutana na post mbalimbali zinazothibitisha dili hilo… ukitembelea page yaTwitter msanii huyo utakutana na tweet moja aliyoshare na mashabiki wake ikisema…
>>> “Signed and Sealed. Meet your latest Adidas ambassador moi… And I’ve got Good news! Stay on this page”… <<< @Peter Okoye.
Peter pia alichukuwa time na kushare good news hiyo na mashabiki wake wa Instagramkwa kupost picha na caption hiyo hiyo kwenye page yake…
Mbali na kuwa balozi wa Adidas, Peter Okoye pia ni balozi wa kampuni ya maziwaNigeria yenye jina ‘Olympic Milk’ na pia staa huyo wa muziki mwenye kipaji kikubwa cha kucheza ameanzisha kipindi chake cha kusaka vipaji kiitwacho ‘Dance with Peter’ambacho kutokana na idadi kubwa ya watazamaji kuongezeka, kipindi hicho kimepata nafasi ya kuonekana kwenye vituo vikubwa, zaidi ya vitano ikiwemo Africa Magic naMTV Base.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni