ENTERTAINMENT
Roma Mkatoliki kwenye
headlines za ualimu, ilikuwa
mwaka gani? stori iko hapa

Najua nina watu ambao mnatamani kufahamu historia za mastaa au changamoto walizokutana nazo kipindi cha nyuma kabla hawajaingia katika tasnia ya Bongo Fleva, sasa stori ninayotaka kukusogezea ni hii kutoka Roma Mkatoliki ambaye amefunguka na kuelezea namna alivyokuwa mwalimu wa sekondari mwaka 2007.
‘Akingea na ripota wa millardayo.com alisema…‘Kipindi chetu sisi tulifeli wengi sana ukiuliza watu wengi waliomaliza kidato cha sita 2007 wengi hawakupa matokeo mazuri kwa hiyo mimi nilienda kusomea Ualimu nipe chaki nipe ubao hautaamini’ – Roma Mkatoliki
‘Kuna baadhi ya mistari yangu ya wimbo wa Tanzania uliokuja baadae unasema kimbilio la waliofeli ni ualimu na polisi ni vitu vilivyotokana na idea kama hizo, mimi nilikuwa nasoma korongwe pale na baada ya muda nikapata ajira kama mwalimu professional na walikuwa wanaangalia masomo niliyofaulu sana ambayo nitakayotumia kuwafundisha wanafunzi mimi nilifaulu Chemistry, Mathematics‘ – Roma Mkatoliki
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni